Mbunge wa Bukoba Mjini, Balozi Khamis Kagasheki(kushoto) ndie alikuwa Mgeni rasmi katika Tamasha la Serengeti fiesta 2014 katika Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba, Tamasha limefanyika usiku wa kuamkia leo. Viongozi mbalimbali wa Serikali, Pamoja na Wananchi mbalimbali walihudhulia kwa wingi katika Uwanja huo wa Kaitaba. katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Bukoa Mheshimiwa Zipporah Pangani na kulia ni Bw. Denis.Mkurugenzi wa Vipindi, Uzalishaji na Mipango wa Clouds Group, Ruge Mutahaba akizungumza jambo na kumkaribisha Mbunge wa Bukoba Mjini, Balozi Khamis Kagasheki jukwaani na kusalimiana na Wakazi wa Bukoba waliokuwa kwenye Tamasha hilo la Serengeti Fiesta 2014 kwenye Uwanja wa Kaitaba.