Pages

Friday, February 28, 2014

MAKOMANDOO,WAZEE WA KIBABA BABA KUPAGAWAISHA BWALO LA POLISI MUSOMA KESHO




Kundi linaloongoza kwa sasa kufanya show kali na kupagawisha watanzamaji kwa kuimba na kuicheza la makomandoo kutoka jijini Dar es salaam linatarajiwa kufanya show kali katika miji ya Musoma,Tarime na Shirati mkoani Mara.

Akizungumza na shommi Blog,muandaaji wa show ambaye pia ni mkurugenzi wa Kayombo Intertainment,Docta Kayombo amesema kwa sasa tayari wasanii hao wameshawasili mjini Musoma tayari kwa kuanza kutoa burudani kwa wakazi wa maeneo hayo.

Kayombo amesema kama ambayo aliwaahidi wakazi wa Musoma na maeneo mengine ya mkoa wa Mara katika show ya usiku wa valentine day ni kuhakikisha wapenzi wa burudani wanapata burudani kila mwishoni mwa wiki baada ya shughuli za kazi.

Amesema show ya kwanza kundio hilo la makomandoo ambalo litasindikizwa na wasanii wengine wakali wa mkoa wa Mara jumamosi ya tarehe 22 watafanya show ya kwanza kwenye ukumbi wa JJ mjini Tarime kabla ya jumapili kufanya show mjini Musoma kwenye ukumbi wa bwalo la polisi klabla ya kumalizia show mjini Shirati jumatatu.

Kayombo amesema baada ya show hiyo ya makomandoo wakazi wa Musoma na maeneo mengine ya mkoa wa Mara watarajie show za wasanii wengine wakali ambao kila wakati watakuwa wakija kutoa burudani kama ilivyo kwenye maeneo mengine.

Saturday, February 15, 2014

HIVI NDIVYO MAMBO YALIVYOKUWA VALENTINE DAY MUSOMA NA KAYOMBO INTERTAINMENT MDANI YA BWALO LA POLISI

 FULL KUJIACHIA
 NI BATA
 ANATAFUTWA MR NA MISS VALANTINE DAY KWA AJILI YA KUJINYAKULIA MPUNGA WA 50,000
 MR VALENTINE AKIFURAHI NA WAPAMBE WAKE

 MSHINDI WA BSS 2013 EMANUEL MSUYA AKITOA BURUDANI
 

 KAYOMBO INTERTAINMENT CLEW
 DOCTA KAYOMBO AKIWA NA MHAZINI MKUU WA KAMPUNI NA KICHUPA MKONONI
 UFATILIAJI
 NIKO NA MKURUGENZI MKUU WA BURUDANI MUSOMA
 MSUYA AKITOA MPUNGA KWA MISS VALENTINE
MPUNGA PIA ULIMUHUSU MR VALENTINE

Mkurugenzi mkuu wa kampuni ya kayombo intertainment,docta Kayombo aaamesema baada ya kupata mafanikio kwenye show ya usiku wa valentine day ndani ya bwalo la polisi mjini Musoma sasa ameamua kuandaa utaratibu wa kuwapa burudani wakazi wa Musoma na mkoa wa Mara kwa ujumla kila mara.

Akizungumza na blog hii,Kayombo amesema kutokana na watu walivyopokea show hiyo anaamini wakazi wa musoma licha ya kujishughulisha na shughuli zao za kiuchumi baada ya kazi wanapenda kujipumzisha na kupata burudani.

Amesema kwa sasa baada ya kuagiza na kufika vyombo vya kisasa vya muziki kilichobaki ni kuhakikisha wakazi wa musoma na vitongoji vyake wanapata burudani nzuri wakati wa mapumziko ya mwisho wa wiki

Tuesday, February 11, 2014

USIKU WA DAYNA NYANGE TZ V/S CINDY SANYU WA UG NDANI YA LINAS NIGHT CLUB BUKOBA FEB 15, 2014


FEB 15, 2014 Itakuwa ni usiku wa aina yake kwa wakazi wa mji wa Bukoba na maeneo ya jirani, Watakapo takiwa kujua nani mkali kati ya DAYNA NYANGE TZ V/S CINDY SANYU WA UG .Usiku huo hatuangalii Vivazi au  nani anamiliki nini,ama yupi ni hot zaidi ya mwenzake,tunaangalia kitu kimoja tu,Nani mkali wa kuimba na kucheza Jukwaani?

Monday, December 16, 2013

TAZAMA PICHA JINSI MSHINDI WA BSS 2013 ALIVYOPOKELEWA MUSOMA KWA SHANGWE




 AMINA CHIBABA AMBAYE NAE ALIINGIA TANO BORA
 ELIZABETH MWAKIJAMBILE AMBAYE PIA ALIINGIA TOP FIVE YA BSS 2013
 NI POZI AMA TEGO
 MOROMORO MAUNO!
 ANAKWAMBIA HAPA KAZI TU.
 WE MAINA
 NI MWENDO WA KIUNO MAUNO WA MSHIRIKI WA BSS 2013 MAINA TADEI
 Dj Mwarabu akiwa mtamboni
 EMANUEL MSUYA AKITOA BURUDANI
 HISIA PIA ZILITAFUTWA
 TWENDE KAZI

 MASHABIKI WA BURUDANI MJINI MUSOMA WAKIMYANYUA JUU KWA SHANGWE EMANUEL MSUYA MSHINDI WA BSS 2013


MSHINDI wa shindano la Bongo Star Search 2013 Emanuel Msuya mwishoni mwa wiki amedhihilishia kwamba hakupendelewa kuibuka mshindi wa shindano hilo baada ya kukonga nyoyo za mashabiki wa burudani mjini Musoma katika show maalumu ya kuwashukuru mashabiki waliopigia kura iliyofanyika kwenye ukumbi wa bwalo la polisi mjini hapa.

Katika show hiyo ambayo Msuya aliambatana na washindi wengine walioiingia tano bora katika kinyang’anyiro hicho,aliwainua mashabiki waliofika katika ukumbi huo mara baada ya kupanda jukwaani na kuanza kuimba wimbo mapenzi wa bendi ya muziki wa dansi ya FM Academmy (Ngwasuma)uliowainua mashabiki wote waliokuwepo ukumbini hapo.

Baada kumaliza kuimba wimbo huo Msuya hakuwarudisha vitini mashabiki pale alipowaendezea shangwe na wimbo wake mpya wa leo ni leo ambao ulionekana kupokewa vyema na mashabiki na kumfanya kila mmoja kutoondoka jukwaani.

Wakizungumza na BLOG hii baadhi ya mashabiki wa burudani walioshuhudia show hiyo ambayo ilionekana kama ya funga mwaka walimuelezea mshindi huyo wa BSS kuwa ni moja ya vipaji ambavyo vilikuwa havionekani na sasa vimeibuliwa.

Walisema Msuya anao uwezo mkubwa wa kulimiliki jukwaa na kuimba na kusema asipoingiza mambo mengine ambayo yamekuwa yakiwapoteza watangulizi wake katika shindano hilo atakuwa ni mmoj ya wasanii watakaofika mbali kwa kufanya vizuri.

Kwa upande wake muandaaji wa burudani hiyo Mkurugenzi wa Kayombe Entertainment&Promotion Dr Theophir Kayombo amewashukuru wakazi wote wa Musoma na maeneo mengine ya nje ya Musoma kwa kumpa mapokezi makubwa mshindi wa BSS 2013 pamoja na washiriki wengine walioingia tano bora alio ambatana nao.

Amesema kwa kuwa ni msimamizi wa wasanii wengi wanaotoka Mkoa wa Mara atahakikisha anamuongoza vyema Msuya ili aweze kufikia kiwango cha juu zaidi na kudai ushauri zaidi wa kujenga kutoka kwa mtu yoyote unapokelewa ili kumjenga msanii huyo.

Washiriki wengine walioambatana na Emanuel Msuya ni Elizabeth Mwakijambile,Maina Tadei,pamoja na Amina Chibaba ambao wote waliimba nyimbo zilizowapa ushindi katika kinyng’anyiro hicho sambasamba na wimbo wa kila mmoja aliorekodi mara baada ya kumalizika kwa shindano hilo.CHANZO SHOMMIBINDA BLOG

Thursday, November 28, 2013

CLUB MODEN KUZINDULIWA IJUMAAA HII MUSOMA USIKOSE






Club Moden at Musoma itafunguliwa rasmi kisho ijumaa chini ya Dj Dady na Max Nx kwa buku kumi tu kuzama mjengoni,Musoma kila siku na mambo mapya

Saturday, October 26, 2013

KIOTA KIPYA SINGITA MARA RIVER







Singita Mara River Tented Camp

We are thrilled to share the first pictures from our brand new camp, Singita Mara River Tented Camp, situated in the Lamai triangle, the northernmost tip of the Serengeti National Park in Tanzania. The camp offers a pared-down approach to the quintessential Singita safari without compromising on any creature comforts.
Singita’s philosophy of preserving iconic locations by offering ‘fewer beds in larger areas’ is epitomised by Mara River Tented Camp’s remote position in the Lamai triangle – with only 16 beds surrounded by 98,000 acres of untouched wilderness.  It is a wildlife viewing area with abundant year-round concentrations of resident plains game, big cats and elephant in addition to the Mara River’s large populations of crocodile and hippo.